Friday, August 12, 2011

FARBEGAS, NASRI NJE LIGI KUU YA UINGEREZA




Klabu ya Arsena imewaondoa Cesc Farbegas na Samir Nasri katika kikosi kitakachocheza na dhidi ya Newcastle siku ya jumamosi katika mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa ligi kuu ya uinegereza.

Farbegas anaeota kutaka kuihama klabu hiyo huku tayari baraca wakitangaza kutoa kiasi cha paundi milion 40 atakosa mchezo huo kutokana na kutokuwa fiti sawasawa kutokana na majeraha yaliyokuwa yakimsumbua kipindi cha nyuma.

Kwa upande wa nasri anaevuma kutimkia Man City, hatokuwemo kutokana na majeraha misuli pamoja na homa aliyopata tokia katika mchezo wa juzi dhidi ya chile aliocheza kwa muda wa dakika 65 na kutolewa.

Venga amekataa kutoa maelezo ya kutosheleza juu ya hatma ya nyota hao na kudai kuwa bado wachezaji wa Arsenal na anajipanga kuhakikisha nyota hao awaondoki.

Ikumbukwe kwamba wiki mbilimzilizopita Venga alinadi kuwa hatama ya farbegas itajulikana mara kabla ya ligi ya uingereza

Kuhusu timu mzee huyo amekiri timu yake inamapungufu baada ya kuwa na majeruhi wengi.

Nyota wengine ambao ni majeruhi katika kikosi hicho ni Jack Wilshere, Laurent Koshien, Theo Walcot, na Robin Van Parse.

Baada ua kurudi St James Park, arsenal itacheza na Liverpool na baadaye Manchester united.

No comments:

Post a Comment